Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, August 22, 2017

RAHEL PALLANGYO APATA TUZO YA MPIGAPICHA BORA




MPIGAPICHA wa Tanzania Standard Newspapers Ltd na Mmiliki wa mtandao huu Rahel Pallangyo amepata tunzo ya mpigapicha bora wa Mashindano ya Ndondo 2017 yaliyofanyika kwenye Mkoa wa Dar es Salaam.
Mbali na tunzo hiyo waandaji wa michuano hiyo walitoa tunzo mbalimbali kwa washindi, tunzo binafsi, vikundi na tunzo za heshima.
Tunzo mwamuzi bora ilichukuliwa na Nadim Mohamed, mwandishi bora alikuwa Charles Abel wa Mwananchi, balozi wa Ndondo mchezaji wa Tottenham ya England Victor Wanyama, shabiki bora alichaguliwa Jata Boy wa Misosi FC na Kitoto cha Ndondo.
Kwa upande wa Wachezaji beki bora alikuwa Kashkash Kindamba wa Keko Furniture, kiungo mshambuliaji bora ni Emanuel Pius kutoka timu ya Goms United, mfungaji bora ni Rashid Roshwa wa Kibada One, mchezaji bora akaibuka Emanuel Memba wa Misosi FC.

Kipa bora ni Haroun Mandanda wa Mlalakuwa Rangers, kocha bora ni Shabani Kazumba wa Goms United, tunzo ya heshima ilitolewa kwa Juma Mwaka na Azam TV na kikundi bora cha ushangiliaji ni Goms United.
Akizungumza baada ya kukabidhi tunzo mgeni wa heshima, Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete alipongeza waandaji wa mashindano hayo kwa kuibua njia mbadala ambayo inawapa fursa wachezaji ambao hawana timu zinazocheza ligi inayotambulika.
“Niwapongeze waandaji kwa kubuni njia mbadala ya kuwapa fursa vijana kuonesha vipaji vyao hivyo naomba mamlaka za zinazosimamia soka kusaidia kuendeleza Ndondo,” alisema Ridhiwani.
Pia Ridhiwani alimpongeza Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Wallace Karia kwa kuchaguliwa kuiongoza TFF na kusema ana imani na uongozi wake.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mjumbe wa Kamati ya utendaji TFF, Elias Mwanjala, mwenyekiti wa Chama cha soka mkoa wa Dar es Salaam, Almas Kasongo, Mwenyekiti wa Chama cha soka Dodoma, Mulamu Nghambi, wadau mbalimbali wa soka, viongozi na baadhi ya wachezaji wa timu zilizoshiriki mashindano hayo.


Balozi wa Ndondo Cup-Victor Wanyama

Mchezaji bora-Emanuel Memba (Misosi FC)


Mfungaji bora-Rashid Roshwa (Kibada One) magoli 6
Balozi wa Ndondo Cup-Victor Wanyama
Kiungo bora-Emanuel Pius (Goms United)
Beki bora-Kash kash Kindamba (Keko Furniture)
Kipa bora-Haroun Mandanda (Mlalakuwa Rangers)
Shabani Kazumba-Kocha Bora (Goms United)
Nadim Mohamed-Mwamuzi bora

Kitoto cha Ndondo-Shabiki bora


Jata Boy-Shabiki bora, Misosi FC
Charles Abel-Mwandishi bora


Tuzo ya heshima-Dr. Mwaka
Tuzo ya heshima-Azam TV

No comments:

Post a Comment