Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, August 20, 2017

DIMBA MUSIC CONCERT KUFANYIKA SEPTEMBA 2 TRAVENTINE


SeeBait
KAMPUNI ya New Habari (2006) LTD kupitia gazeti lake la DIMBA, imeandaa onesho maalum la muziki wa dansi DIMBA Music Concert litakaofanyika Septemba 2 mwaka huu katika Ukumbi wa Traventine Magomeni jijini Dar es Salaam.
Onesho hilo lina lengo la kuukuza na kupromoti muziki wa dansi ambao umekuwa ukielekea kupotea kila kukicha.
Katika onesho hilo kutakuwepo na mpambano wa wanamuziki wa dansi, ambapo bendi ya Msondo Ngoma Music (Baba wa Muziki), itachuana na mastaa mbalimbali wa muziki huo kutoka bendi mbalimbali nchini.
Kundi la mastaa ambao wamepewa jina la ‘Timu ya Taifa ya Muziki wa Dansi,’ litakalochuana na Msondo Ngoma, litaundwa na wanamuziki kama Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kiki’, Hassan Rehani Bitchuka ‘Stereo’, Karama Regesu, Ally Choki, Juma Kakere, Nyoshi El-Saadat ‘Sauti ya Simba’ na Muumini Mwinjuma.
Mhariri wa Dimba, Jimmy Chika, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanamuziki na wajumbe wa kamati ya maandalizi ya Dimba Concert
Kwa upande wa vyombo, watakuwepo wapiga vyombo Saadi Ally ‘Machine’ kwenye dramu, gitaa la solo litapigwa na Aldofu Mbinga wakati besi litangurumishwa na Hosea Mhogachi.
Aidha, kinanda kitapapaswa na Juma Jerry wakati tumba zikikung’utwa na Salum Chakuku ‘Kuku Tumba’, ambapo ala za upepo watakuwepo Ally Yahaya, Hamis Mnyupe Tarumbeta na Shaabani Lendi kwenye Saksafoni.
“Utakua ni usiku wa mastaa wa dansi kuionyesha kazi Msondo Ngoma, kwani miaka ya hivi karibuni imekua ikikosa mbabe katika kila bendi inayoshindanishwa nayo lakini safari hii tumeamua tuwaonyeshe kazi,”alisema meneja matukio wa Dimba Music Concert, Mwani Nyangassa. 
Kiingilio katika onesho hilo litakaloanza kuanzia saa 2:00 usiku hadi majogoo, kitakuwa ni shilingi 10,000 kwa wote na 20,000/- kwa VIP.

No comments:

Post a Comment