UJIO
wa Kocha Sue Purchase kutoka katika shule ya kimataifa ya Mtakatifu Felix
Uingereza kusaka vipaji vya mchezo wa kuogelea kwenye mashindano ya taifa
kutawanufaisha wachezaji watakaoonyesha uwezo.
Mashindano
ya klabu bingwa Taifa yanatarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii na
kushirikisha wachezaji 172 kutoka klabu 15 za Tanzania bara na Zanzibar.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA) Ramadhan Namkoveka, Purchase ambaye pia ni Mkurugenzi wa michezo wa kuogelea wa shule hiyo, lengo ni kusaka vipaji vya mchezo huo.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA) Ramadhan Namkoveka, Purchase ambaye pia ni Mkurugenzi wa michezo wa kuogelea wa shule hiyo, lengo ni kusaka vipaji vya mchezo huo.
“Wachezaji
Sonia Tumiotto, Collins Saliboko, Anjani Taylor, Smriti Gokarn na
Aliasgar Karimjee ambao wanasoma Uingereza tayari wameshawasili nchini kushiriki
mashindano ya Taifa na wanaendelea na mazoezi ya Dar es Salaam,” alisema.
Namkoveka alisema kuwa waogeleaji wameonyesha viwango vya hali ya juu kiasi cha kumfanya Purchase kuamua kuja nchini kushuhudia waogeleaji wengine wa Tanzania katika mashindano hayo
Namkoveka alisema kuwa waogeleaji wameonyesha viwango vya hali ya juu kiasi cha kumfanya Purchase kuamua kuja nchini kushuhudia waogeleaji wengine wa Tanzania katika mashindano hayo
Alisema
kuwa mbali ya kushuhudia mashindano hayo na kusaka vipaji, kocha huyo atakutana
na wazazi, makocha, waogeleaji wa klabu ya Dar Swim Club na kufanya nao
mazungumzo.
Alisema kuwa hii ni faraja kwa wadau, wachezaji, Klabu na viongozi wa mchezo wa kuogelea kwani ujio wa kocha ni ishara ya mchezo kukua.
Alisema kuwa hii ni faraja kwa wadau, wachezaji, Klabu na viongozi wa mchezo wa kuogelea kwani ujio wa kocha ni ishara ya mchezo kukua.
Mashindano
hayo yatashirikisha klabu 15 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambazo zitashindana
katika staili za backstroke, freestyle, breaststrokes, Butterfly na Individual
Medley (IM).
No comments:
Post a Comment