WAKATI
wenzake wakipandishwa kizimbani juzi wakituhumiwa na kesi za dawa za
kulevya, Wema Sepetu ameendelea kusota
rumande kwa matumizi ya simu ya mkononi huku akiwa ameshikiliwa na jeshi la
Polisi.
Hayo
yalisemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kudai ni
makosa katika nchi hii ukiwa yupo chini ya ulinzi halafu kuendelea kutumia simu
ya mkononi.
“Matumizi ya
simu watu wakiwa gerezani yamekuwa yakitumika kuendeleza biashara za dawa za
kulevya kwa njia ya mawasiliano hata kama wakiwa ndani,” alisema Makonda.
Makonda
alisema amezungumza na wakuu wa Magereza yote yaliyopo Dar es Salaam na
wakuu wa mikoa juu ya vitendo vya watu kuingia na simu katika vituo vya polisi.
Wema alikuwa akituma Video na sauti mbalimbali kuhusu hali ya maisha akiwa mahabusu ya kituo cha kati huku akimkejeli mkuu wa mkoa hivyo huenda akaendelea kuwa katika wakati mgumu kutokana na kitendo hicho cha kutumia simu akiwa mahabusu.
Wema alikuwa akituma Video na sauti mbalimbali kuhusu hali ya maisha akiwa mahabusu ya kituo cha kati huku akimkejeli mkuu wa mkoa hivyo huenda akaendelea kuwa katika wakati mgumu kutokana na kitendo hicho cha kutumia simu akiwa mahabusu.
No comments:
Post a Comment