Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, April 8, 2018

TWIGA STARS YATOKA SARE, YAAGA MASHINDANO





TIMU ya Wanawake  ya Soka ya Tanzania Twiga Stars, imeaga mashindano ya Afrika kwa wanawake baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Nkoloma Lusaka Zambia.
Mchezo huo wa kutafuta kufuzu fainali za Afrika zinazotarajiwa kufanyika Ghana kuanzia Novemba 17 hadi Desemba Mosi mwaka huu jahazi la Twiga lilionekana kuanza kuzama mapema baada ya kukubali bao la mapema.
Wenyeji She Polopolo walipata bao dakika ya tatu lililofungwa na Rachael Kundanaji baada ya kumzidi mbio beki Sophia Mwasikili na kudumu hadi mapumziko licha ya kutawala mchezo kipindo chote hicho.
Twiga Stars ambao walitawala mchezo kipindi cha pili walisawazisha bao hilo dakika ya 71 ambalo lilifungwa na mshambuliaji Donisia Daniel akiunganisha kona iliyopigwa na Mwanahamisi Omar ’Gaucho’
Kwa matokeo hayo Zambia wamefuzu hatua ya pili kwa ushindi wa mabao 4-4 baada ya kutoka sare ya mabao 3-3 nyumbani na sasa itakutana na mshindi kati ya Zimbabwe au Namibia.
Twiga Stars iliwahi kufuzu fainali hizo 2010 ambazo zilifanyika nchini Afrika Kusini na kutolewa katika hatua ya makundi.



No comments:

Post a Comment