TAMASHA la
Sauti za Busara 2017, Ijumaa litaendesha mafunzo ya sanaa inayohusu fursa za
mitandaoni, changamoto na vitisho vinavuyoigusa tasnia ya muziki.
Akizungumza
na gazeti hili Mkurugenzi wa tamasha la Sauti za Busara Bw.Yusuf Mahmoud
alisema kwa kutambua uwezo wa kidigitali ni muhimu kwenye taaluma, wahudhuriaji
wakajifunza nguvu ya mitandao ya kijamii
ilivyo na nguvu ya kuunganisha mashabiki na wawekezaji, na kuongeza masoko kwa
kutumia mitandao ya kijamii.
“Wanamuziki hujikuta mstari wa mbele kwenye harakati kwa kutumia sauti zao kwa niaba ya wasiosikika wakati mwingine wasanii hujikuta hatarini baada ya ujumbe wa muziki wao kuwatuhumu wasikilizaji na wenye mamlaka,” alisema Mahmoud.
“Wanamuziki hujikuta mstari wa mbele kwenye harakati kwa kutumia sauti zao kwa niaba ya wasiosikika wakati mwingine wasanii hujikuta hatarini baada ya ujumbe wa muziki wao kuwatuhumu wasikilizaji na wenye mamlaka,” alisema Mahmoud.
Pia Mahmoud alisema msanii anaweza kutumia uhuru wa kuongea
na kufungiwa kitaaluma ni mada ambayo itaeleza mtazamo huru wa ubunifu
Afrika.
Jumapili wasanii wanakaribishwa kwa maswali na majibu ya kina na ni sehemu ya kipekee kwa wasanii kutoka bara la Afrika na sehemu mbalimbali kukutana na kubadilishana mawazo.
Jumapili wasanii wanakaribishwa kwa maswali na majibu ya kina na ni sehemu ya kipekee kwa wasanii kutoka bara la Afrika na sehemu mbalimbali kukutana na kubadilishana mawazo.
Kuingia ni kwa mwaliko tu hivyo wasanii na mameneja wa
ndani wanahamasishwa kuwasiliana na waandaaji wa tamasha la
Sauti za Sauti za Busara kama watapenda kushiriki.
Tamasha la Sauti za Busara 2017 linatarajiwa kuanza leo hadi Februari 12 Mji Mkongwe, Zanzibar.
Tamasha la Sauti za Busara 2017 linatarajiwa kuanza leo hadi Februari 12 Mji Mkongwe, Zanzibar.
No comments:
Post a Comment