Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, February 14, 2017

SERENGETI BOYS KUTEMBELEA SOBER HOUSE BAGAMOYO





KATIKA kuhakikisha inapiga vita matumizi ya madawa ya kulevya Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) limeandaa ziara ya mafunzo kwa timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ‘Serengeti Boys’ ili kuwaepusha na janga hilo.
Akizungumza na wandishi wa habari jana, Ofisa habari wa TFF, Alfred Lucas alisema Machi 4 watafanya ziara ya kutembelea Sober house ya Life and Hope iliyopo Bagamoyo Pwani ili wachezaji hao wakajionee jinsi madawa ya kulevya yanavyaathiri.
“Unajua wachezaji wa Serengeti boys wapo kwenye hatua ya mabadiliko ya kimwili ambayo huleta vichocheo vingi ambavyo husababisha kujiingiza kwenye makundi na tabia mbaya,” alisema Lucas.
Pia Lucas alisema wachezaji hao ambao wataandamana na waandishi wa habari watawapelekea zawadi vijana wanaotibiwa kwenye kituo hicho ili nao wajione ni sehemu ya jamii na kuonyesha kuwa wameguswa na janga hilo pamoja na kushiriki katika jitihada za Serikali za kuthibiti matumizi ya dawa za kulevya.
“Vijana wa Serengeti nao wanakuwa sasa, wanatamani kujaribu vitu vingi, wanataka kuwa na wapenzi kufanya mambo mbalimbali kwakuwa wanajiona ni wakubwa kwahiyo tutawapeleka Bagamoyo ili wakajionee madhara yatokanayo na matumizi ya dawa za kulevya” alisema Lucas.
Suala la madawa ya kulevya ni vita ya kila mtu hivyo TFF imeunga mkono serikali kuhakikisha vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa haijiingizi kwenye matumizi ya dawa za kulevya

No comments:

Post a Comment