Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, December 1, 2016

SHIME NDANI YA JKT RUVU



KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 'Serengeti Boys' Bakari Shime amekabidhiwa mikoba ya kuinoa JKT Ruvu kuanzia mzunguko wa pili wa ligi kuu utakaoanza Disemba 17.
 Shime anachukua nafasi ya kocha Malale Hamsini ambaye alianza kuifundisha timu hiyo mwanzoni mwa msimu huu akitokea Ndanda FC.
Akizungumza na gazeti hili Ofisa Habari wa JKT Ruvu, Constantine Masanja alisema uongozi umeamua kufanya marekebisho kwenye benchi la ufundi ili kuhakikisha wanafanya vizuri baada ya mzunguko wa kwanza kumaliza wakiwa nafasi ya 14  huku wakiwa na pointi 13.
"Uongozi umefanya mabadiliko kwenye benchi la ufundi sasa kocha mkuu ni Shime akisaidiwa na Mwamgaya pamoja na Sajini Abdallah," alisema Masanja.
Masanja alisema usajili uongozi umemuachia kocha Shime kuamua kupunguza au kuongeza wachezaji kabla ya kufungwa dirisha la usajili, Disemba 15
Ruvu wameingia kambini Novemba 25 kujiandaa na mikikimikiki ya duru la pili  kwenye Uwanja wa JKT Mbweni chini ya kocha huyo wa zamani wa Mgambo JKT ya Tanga ambayo sasa inashiriki Ligi Daraja la Kwanza.

No comments:

Post a Comment