Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, August 1, 2016

TIMU YA RIADHA INAYOKWENDA MASHINDANO YA OLIMPIKI YAAGWA LEO



 pix 6 b
Wanamichezo nchini wameaswa kutojihusisha na matumizi ya dawa au mbinu za kuongeza nguvu katika michezo ili kuepuka na madhara yanayojitokeza ikiwemo kuzorotesha sekta ya michezo.
Wito huo umetolewa leo na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura alipokuwa akiwaaga wanamichezo wanaoenda kushiriki mashindano ya Olimpiki kwa mwaka 2016 yanayofanyika Jijini Rio dejaneiro nchini Brazil.
Mhe. Anastazia Wambura amesema kuwa wanamichezo wengi duniani kwasasa wanakabiliwa na changamoto kubwa ya matumizi ya dawa na mbinu za kuongeza nguvu mwilini katika michezo mbalimbali.
“Niwatake wachezaji,madaktari na viongozi wa michezo mbalimbali kuhakikisha kuwa hakuna mchezaji anajejihusisha na vitendo vya aibu na kwa pamoja tuungane na kupinga jambo hili kwa kujali afya na ushindani uliopoa” alisema Mhe. Anastazia.
Aidha amewataka viongozi wote wa michezo, waalimu na madaktari wa michezo kuungana kwa pamoja kupiga vita matumizi ya dawa za kuongeza nguvu michezoni kwa kutoa elimu kwa wanamichezo wao na wasisite kutoa adhabu kali pale inapothibitika mwanamichezo amejihusisha na matumizi ya dawa hizo.
Kwa upande wake katibu wa kamati ya Olimpiki Tanzania Filbert Bayi ameahidi kutekeleza suala hilo kwa kutoa elimu kwa waalimu na wanamchezo juu ya madhara ya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu za mwili katika michezo.
                                                                                                                                     

No comments:

Post a Comment