Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, July 29, 2016

MO AITAKA SIMBA KWA BILIONI 20



MFANYABIASHARA maarufu nchini, Mohammed Gulam Dewji ama 'MO' amesema yupo tayari kufanya uwekezaji wa bilioni 20, Simba endapo tu wanachama wa klabu hiyo wataridhia mpango wake.
Mo amekuwa akihusishwa kutaka kufanya uwekezaji mkubwa ndani ya Simba huku baadhi ya wanachama wa klabu hiyo wakionekana kutokuwa tayari kutokana na sababu zao binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Dar es Salaam leo MO amesema kinachomvutia kufanya uwekezaji huo mkubwa kwa Simba ni mapenzi aliyonayo kwa klabu hiyo.

 "Naipenda Simba toka moyoni,niliwahi kuidhamini miaka ya nyuma na tulifanya vizuri sana katika michuano ya kimataifa kila mwanasimba analijua," amesema MO.

Wakati huohuo Mo amesema bajeti ndogo ya Simba ndiyo inayoifanya klabu hiyo kushindwa kushindana vizuri katika soko la usajili na klabu za Yanga na Azam.

Mo ameongeza kuwa endapo atapewa ridhaa ya kufanya uwekezaji basi ndani ya miaka mitatu ataijengea klabu hiyo kiwanja bora cha mpira, hosteli, Gym na kuajiri makocha wenye vigezo.

Simba inatarajiwa kufanya mkutano mkuu wa wanachama utakaojadili juu ya uendeshwaji wa klabu hiyo siku ya Jumapili katika Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay



No comments:

Post a Comment