Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, March 2, 2015

CHELSEA WAIBUKA MABINGWA WA CAPITAL ONE CUP BAADA YA KUIFUNGA TOTTENHAM MABAO 2-0

CHELSEA leeo hii Uwanjani Wembley Jijini London wametwaa Taji la kwanza la Msimu, likiwa Kombe la kwanza kwa Meneja wao Jose Mourinho tangu 2012, walipoichapa Tottenham Bao 2-0 katika Fainali ya Kombe la Ligi huko England ambalo sasa linaitwa Capital One Cup.
Kipindi cha Kwanza Tottenham walitawala lakini Chelsea walipata Bao lao la Kwanza Dakika ya 45 kutokana na Frikiki ya Willian kushindwa kuokolewa na Beki wa Spurs Danny Rose ambae Kichwa chake duni kilimfikia John Terry aliepiga Mpira uliomgonga Harry Kane na kumbabaisha Kipa wao Hugo Lloris na kutinga.
Dakika ya 56 Chelsea walipata Bao lao la Pili baada ya Shuti la Diego Costa kumbabatiza Beki wa Spurs Kyle Walker na kumhadaa Kipa Hugo Lloris.
Kwa kutwaa Capital One Cup Chelsea wanahakikishiwa kucheza Ulaya Msimu ujao kwenye UEFA EUROPA LIGI lakini kama watamaliza kwenye 4 Bora za Ligi Kuu England watacheza UEFA CHAMPIONS LIGI badala yake.

No comments:

Post a Comment