Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, October 23, 2014

KOCHA WA BARCELONA FC, LUIS ENRIQUE TUMBO JOTO! KUELEKEA MCHEZO WA "EL CLASICO" WA JUMAMOSI DHIDI YA REAL MADRID, ASEMA MATOKEO YOYOTE KWAO NI SAWA.


JUMAMOSI ndio Siku ambayo Vigogo wa Soka huko Spain, Real Madrid na FC Barcelona, watakapocheza Mechi yao ya kwanza ya La Liga Msimu huu Uwanjani Santiago Bernabeu kwenye pambano ambalo hubatizwa Jina rasmi ‘El Clasico.’
Safari hii, licha ya kuwapambanisha wale Masupastaa bora Duniani, Cristano Ronaldo, ambae ndiie rasmi Mchezaji Bora Duniani, na Lionel Messi, pia atakuwepo Mfungaji Bora Duniani, James Rodriguez, alietwaa Buti ya Dhahabu ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil, akiichezea Real Madrid katika El Clasico yake ya kwanza.
Kivutio kingine, akicheza El Clasico yake ya kwanza, ni Straika mpya wa Barcelona, Luis Suarez, ambae hii huenda ikawa ni Mechi yake ya kwanza rasmi kuichezea Barca baada ya kumaliza Kifungo chake cha Miezi Minne alichopewa huko Brazil Mwezi Juni baada ya kumng’ata Beki wa Italy, Giorgio Chellieni, kwenye Mechi ya Fainali za Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment