Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 31, 2013

NEYMAR KUONEKANA BARCELONA MARA YA KWANZA LEO, BARCA WAKIUMANA KWENYE MECHI YA KIRAFIKI NA LECHIA GDANSK


MCHEZAJI MPYA Neymar, ataonekana kwa mara ya kwanza ndani ya Jezi ya Barcelona Uwanjani huko Poland wakati Mabingwa hao wa Spain watakapocheza Mechi ya Kirafiki na Lechia Gdansk Siku ya Jumatano.
Mechi hii ilikuwa ichezwe mapema Mwezi huu lakini ilifutwa mara baada ya kutangazwa kuondoka kwa Meneja wa Barcelona, Tito Vilanova, kwa matatizo ya maradhi ya Kansa.
Kikosi ambacho kitacheza huko Poland kina Vijana wengi lakini pia wapo Lionel Messi, Cristian Tello na Alex Song na kitaongozwa na Kocha Msaidizi, Jordi Roura, huku Kocha mpya Tata Gerardo Martino akibaki Barcelona na Wachezaji wengi wa Timu ya Kwanza waliochelewa kurudi Mazoezini baada ya kuongezewa Likizo kwa vile walicheza Kombe la Mabara huko Brazil Mwezi uliopita.
Neymar wakati anatambulishwa Barca siku za nyuma kidogo 

No comments:

Post a Comment