Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 31, 2013

RATIBA SERIE A MSIMU WA 2013/14 HA!! MABINGWA JUVE KUANZA UGENINI NA SAMPDORIA!!



Juventus wakishangilia RATIBA ya Msimu mpya wa Ligi ya Italy, Serie A, imetoka na Mechi za ufunguzi ni Wikiendi ya Agosti 24 na 25 na Mabingwa Watetezi Juventus wataanza ugenini na Sampdoria, Timu pekee ambayo iliwafunga nje ndani Msimu uliopita.Ligi hiyo itamalizika hapo Mei 18 Mwaka 2014.
Ratiba hiyo, iliyoandaliwa na Kompyuta, ilitolewa leo huko Mjini Milan katika sherehe maalum.
Katika Msimu huu mpya zipo Dabi 5 za Miji ya Milan, Rome, Turin, Genoa na Verona lakini Ratiba zake zimehakikisha Mechi zake hazipangwi katikati ya Wiki kwa sababu za Kiusalama.
Pia, Klabu ambazo zimo Mashindano ya UEFA, CHAMPIONZ LIGI na EUROPA LIGI, zimetenganishwa zisikutane zile Wiki kabla ya Mechi zao za UEFA. 

No comments:

Post a Comment