Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, November 16, 2015

TIMU YA ALLIANCE YA MWANZA YAANZA LIGI VEMA, HUKU COSMOPOLITAN IKITOKA SARE NA KARIAKOO YA LINDI

Ligi Daraja la Pili nchini (SDL) imeanza kutimua vumbi jana katika viwanja 12 mikoa mbali, huku timu 24 zikisaka nafasi nafasi nne za kupanda Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao wa 2016/2017.
Katika michezo iliyochezwa jana matokeo yalikuwa ni Alliance 2 -0 Madini, JKT Rwamkoma 1- 3 Bulyanhulu, Mvuvuma 0 – 0 Green Warriors, Singida United 1 -0 Transit Camp, Mirambo 1 – 0 Abajalo Tabora.
Karikaoo 1 – 1 Cosmopolitan, Mshikamano 1- 1 Changanyikeni, Villa Squad 0 – 2 Abajalo Dar es salaam, Mkamba Ranger 0 -0 The Mighty Elephant, Sabasaba 0 - 1 Mbeya Warriors, Wenda 0 – 0 African Wanderes.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea Novemba 28, kwa timu 24 kucheza katika viwanja 12 mbalimbali nchini kusaka pointi muhimu.

No comments:

Post a Comment