Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, November 19, 2015

SIMBA YAMPA SHAVU BRIAN MAJWEGA, ANAANZA MAZOEZI RASMI CHINI YA KERR

MAJWEGA (KULIA) WAKATI AKIWA AZAM FC, AKIPAMBANA NA JUMA ABDUL WA YANGA.

Taarifa kwa vyombo vya habari
Simba Sports Club
Dar es salaam
18-11-2015

Klabu ya Simba inapenda kuwafahamisha kuwa imeridhia ombi la kufanya mazoezi na timu yetu toka kwa mchezaji wa kimataifa wa Uganda, Brian Majwega.
Ombi hilo la Majwega limekuja kwetu ili apate kujiweka fit. Ukizingatia kazi rasmi ya mchezaji huyo ni kucheza mpira wa miguu
Kwa sasa mchezaji huyo ana mgogoro na klabu yake ya zamani timu ya Azam FC ya jijini Dar es salaam
Katika barua yake kwa klabu ya Simba ambayo nakala yake imetumwa shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF. Majwega ameomba kujumuika na timu yetu ukizingatia uwepo wa wachezaji wengine wa kiganda Juuko Murshid na Hamis kiiza
Kesho alhamis tarehe 19-11-2015 Majwega ataanza rasmi mazoezi na klabu yetu.chini ya kocha Kerr jijini Dar es salaam
Imetolewa na
Haji S Manara
Mkuu wa mawasiliano
Simba sports club
Simba nguvu moja
Kwa hisani ya Saleh Jembe blog

No comments:

Post a Comment