Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, July 31, 2015

OLYMPIKI MAALUM YAPATA MEDALI ZA DHAHABU KWENYE RIADHA

Mwanariadha Blandina Patrick ambaye alishika nafasi ya kwanza kwenye mbio za mita 800 na kupewa medali ya dhahabu akiwa na wenzake baada ya kuvalishwa medali kwenye mashindano ya dunia ya Olympiki maalum yanayofanyika nchini Marekani. (Picha na Mpiga picha wetu)

Blandina Patrick


WANARIADHA watano wa timu ya Olimpiki Maalum inayoshiriki mashindano ya dunia yanayofanyika Marekani wamepata medali.

Akizungumza kwa njia ya mtandao kutoka Los Angels, Marekani jana, Mkuu wa msafara, Frank Macha alisema Tanzania imeendelea kujinyakulia medali baada ya juzi kupata medali tatu.

Wachezaji wetu wamefanikiwa kupata medali nyingine tano baada ya zile tatu ambazo zilinyakuliwa  awali. Waliopata medali ni Blandina Patrick amepata medali ya dhahabu  na Deonatus Manyama  medali ya fedha wote  kwenye mbio za mita 800.

Wengine ni  Faraja Meza  aliyepata medali ya dhahabu, Riziki Chilumba medali ya fedha na Aisha Kaoneka  medali Shaba kwenye mbio za mita 100 wote.

Wachezaji wengine ambao walishajinyakulia medali ni Godfrey Jabuya, Blandina Patrick na Deonatus Manyama kwenye mbio za mita 400 hivyo hadi sasa Tanzania imefikisha jumla ya medali nane, dhahabu tatu, fedha tatu na shaba  mbili

Timu hiyo ina wachezaji wanane, wanawake wanne na wanaume wanne, itashiriki katika mchezo wa riadha katika mita 100, 200, 400, 800, 5000, nusu marathon na mita 4x100 kupokezana vijiti. (Relay).

No comments:

Post a Comment