Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, March 10, 2015

WAHADHIRI UDSM KUTUNUKIWA VYETI VYA UKOCHA NA KIFA


Mkufunzi George Komba (kulia) na Oscar Mirambo na Mhadhiri wa UDSM Albert Kimaro wakiteta jambo


Wana kozi ya awali ya ukocha inayoendeshwa na KIFA kwenye viwanja vya Chuo Kikuu

Mhadhiri wa UDSM, Albert Kimaro akifundisha kwa vitendo wakati wa kozi ya awali ya ukocha inayofanyika Viwanja vya chuo hicho



WAHADHIRI wawili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wanatarajia kufuzu mafunzo ya awali kozi ya ukocha inayoendeshwa na Chama cha Soka, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Waadhiri hao ni Noel Kiunsi Albert Kimaro ambao wote wapo Idara ya Physical Education ya Chuo hicho.
Akizungumza wakati wa mazoezi ya vitendo yanayofanyika kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu, Noel Kiunsi alisema kuwa ameamua kujiunga na kozi hiyo ili apate nafasi ya kufundisha vilabu vya mtaani kwani kutokana na kanuni za Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) hazitambui watu wenye shahada ya michezo kama ilivyo wao.
“Mimi nin shahada ya michezo lakini siwezi kufundisha timu zinazoshiriki ligi ya TFF bila kuhudhuuria kozi ambazo wanaendesha wao ndo maana nimejiunga ili nitumie ujuzi hadi nje ya chuo”, alisema Kiunsi.
Kozi  ambayo imeandaliwa na Chama cha Soka Mkoa wa Kisoka Kinondoni (KIFA) inafundishwa na Mkufunzi George Komba toka Dodoma akisaidiana na Oscar Mirambo.
Jumla wa makocha 23 wanatajia kutunikiwa vyeti vya awali endapo watafauli mitihani ya nadharia na vitendo kwenye kozi hiyo ambayo ilianza Februari 16 na inatarajiwa kumalizika kesho.

No comments:

Post a Comment