Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, March 10, 2015

TFF YAWEKA HADHARANI AGENDA ZA MKUTANO MKUU WA MOROGORO


Rais Malinzi akiongea na wandishi kushoto ni Mkurugenzi wa Mashindano, Boniface Wambura na kulia ni mshauri wa rais wa mambo ya ufundi


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetoa agenda za mkutano wake Mkuu utakaofanyika mjini Morogoro kati ya Machi 14,15 mwaka huu katika Ukumbi wa Morogoro Hotel

Akizungumza na wandishi wa habari , Afisa habari wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Baraka Kizuguto alisema kuwa mkutano utafanyika mjini Morogoro na mandalizi yanaendelea vizuri

“Kama mnavyojua TFF itafanya mkutano wake Mkuu Machi 14 na 15 mwaka huu mjini Morogoro na maandalizi yanaendelea vizuri”, alisema Kizuguto.

Agenda za mkutano mkuu ni kufungua Mkutano, uhakiki wa Wajumbe,  kuthibitisha Ajenda, kuthibitisha Muhtsari wa Mkutano Mkuu uliopita na yatokanayo na Mkutano uliopita.
Nyingine ni hotuba ya Rais, ripoti kutoka kwa Wanachama, kuthibitisha ripoti ya utekelezaji wa Kamati ya Utendaji, kuthibitisha ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu 2013.
Pia kutakuwepo na agenda ya kuthibitisha ripoti ya Kamati ya Ukaguzi wa Hesabu, kupitisha bajeti ya 2015, marekebisho ya Katiba, mengineyo na mwisho ni kufunga Mkutano.
Awali Mkutano huu ulikuwa ufanyike mkoani Singida lakini ulihamishwa kutokana na mkoa huo kutokuwa na hoteli za kukidhi mahitaji ya wajumbe na gharama kuwa juu.
    

No comments:

Post a Comment