Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, February 17, 2014

KINDA LA SERENGETI BOYS LAPATA TIMU THAILAND



 Photo: ซุบตาร์กบินทร์
WINGA machachari wa Polisi Dar es Salaam inayocheza Ligi daraja la kwanza Tanzania Bara, Hamis Mroki amefuzu majaribio nchini Thailand kwenye timu ya Kabin United.

Mroki ambaye amewahi kuchezea Mtibwa na timu  za Taifa za vijana Serengeti boys na Ngorongoro heroes ‘U-23’ amefuzu kuchezea timu hiyo ya daraja la pili baada ya kufanya majaribio kwa siku mbili badala ya siku 30 kama walivyokubaliana na timu hiyo.

Pia anasema kocha wa timu hiyo alivutiwa naye baada kuona ana uwezo wa kucheza nafasi nyingi kitu ambacho ni nadra kwa wachezaji wengi.

“Nilikuwa nifanye majaribio kwa siku 30 lakini nashukuru baada ya siku mbili nilifuzu kutokana na kiwango changu kumridhisha kocha na sasa ndio nafuatilia Uhamisho wa Kimataifa hapa TFF ili niondoke”, alisema Mroki

Mroki anacheza namba 7, 8, 11 na wakati mwingine namba 10 kutokana na mfumo wa timu utakaokuwa unacheza.

Pia alisema Polisi Dar imekubali aondoke kwani awali walikubaliana akipata timu nje ya nchi watamruhusu kuondoka na amelishukuru Shirikisho la Soka Tanzania kwa kumpatia ICT ili aweze kuendeleza kipaji chake.

No comments:

Post a Comment