Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, February 17, 2014

SIKINDE YAREKODI UYA WIMBO WA 'DUNIANI KUNA MAMBO' KWA KUMSHIRIKISHA LADY JAY DEE



 
BENDI ya Sikinde jana ilifanya kazi ya kurekodi upya wimbo wa ‘duniani kuna mambo’ na kumshirikisha mwanadada Lady Jay dee.

Wimbo huo wa Sikinde umerekediwa katika studio za FM zilizopo jijini Dar es Salaam
Katika wimbo huo Lady Jay Dee ameshiriki kuimba kipande la mwanzo kabisa kisemacho "Duniani kuna mambo" kabla ya Bitchuka kuimba  pande la pili lisemalo "hata ukifanya jambo Zuri"

Kwa upande wa kibwagizo kimenogeshwa na Mzee mzima Muhidin Gurumo na kwa upande wa  gitaa la Solo kasimama Mapesa, Maufi kwenye Rythm na Mbwana Mponda kapiga bass.

Akizungumzia jijini, Msemaji wa Bendi hiyo Jimmy Chika alisema kuwa wimbo huo utaanza kusikika katika vituo mbalimbali vya radio kuanzia jumatatu.

“Wimbo huo umeshakamilika na utaanza kusikika kote nchi nzima kwenye radio na tupo kwenye mkakati wa kurekodi upya nyimbo zingine sita kwani tunataka kabla ya kumwaga mzee Gurumo hiyo kazi iwe imekamilika”, alisema Chika

Sikinde ni moja ya bendi kongwe hapa nchini ambazo zimekuwa zikitunga na kuimba nyimbo zenye kuleta maana kwa jamii.

No comments:

Post a Comment