Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, October 22, 2013

KALABA, SUNZU NA SINKALA WAREJESHEWA PASSPORT ZAO

Serikali ya Zambian imewarejeshea pasi za kusafiria wachezaji watatu wa TPN Mazembe Rainford Kalaba, Stoppila Sunzu na Nathan Sinkala, na hivyo kumaliza mzozo ulioibuka kufuatia kushindwa kuungana na wenzao katika michezo miwili ya kimataifa.
Zambia iliwanyang'anya wachezaji hao pasi zao za kusafiria baada ya kushindwa kuelekea Beijing kwa ajili ya mchezo wa kimataifa dhidi ya Brazil nchini China wiki iliyopita ambapo sasa maafisa wa uhamiaji wamewarejeshea pasi zao na kwasiri vijana hao wamerejea katika klabu yao ya TP Mazembe ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Hta hivyo hii leo, Kalaba na Sunzu wamechukua makabrasha yao ilhali Sinkala akitakiwa kuchukua kutoka katika ofisi za uhamiahi za mjini Ndola.

No comments:

Post a Comment