Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, July 4, 2013

YOUNG COACHES YAZIDI KUTAKA HUKU WAKONGWE WAKIWAFUNZA VIJANA JINSI YA KUSAKATA KABUMBU

TIMU ya Young Coaches jana iliifunga New Eleven bao 1-0 kwenye mchezo wa kombe la ng’ombe uliochezwa Uwanja w Beira Msimbazi, Ilala

Mchezo huo ambao ulisheheni wachezaji wa zamani ambao ndio wanaounda timu ya Young Coaches ulihudhuriwa na umati mkubwa.

Young Coaches walijipatia bao dakika ya 27 kupitia kwa mshambuliaji wao wa Kimataifa wa Nigeria George Anyanwu baada ya kuunganisha pasi ya Shafii Dauda.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko hata hivyomabadiliko hayo hayakuweza kubadilisha matokeo ya kipindi cha kwanza.

Akizungumza baada ya mchezo, nahodha wa Young Coaches, Mohamed Husein “mmachinga” alisema kuwa mchezo ulikuwa mzuri ila timu yao haina mazoezi ya kutosha zaidi uzoefu ndio unawasaidia wasifungwe.

“Timu yetu hatuna mazoezi ya pamoja ndio maana tunashindwa kufunga mabao mengi kwa sababu ya kukosa pumzi ila uzoefu ndio unatubeba”, alisema Mohamed

Kikosi cha Young Coaches kilikuwa na Moses Mkandawile, Shedrack Nsajigwa, Mwanamtwa Kihwelo, Athuman Kipao, Zuberi Katwila, Shafii Dauda, George Anyanwu, Edibily Lunyamila, Emanuel Gabriel, Shomari Chaurembo na Grayson Swai

Wengine ni Steven Nyenge, Ally Yusufu ‘Tigana’, George Lucas, Zulfikri Idd, Collin Frich na Omari Mbarouk







No comments:

Post a Comment