Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, July 4, 2013

TAIFA STARS YAANZA MAZOEZI LEO, KIKOSI CHOTE KIPO KAMILI KUIVAA UGANDA JULAI 13

TIMU ya Taifa ‘Taifa Stars’ jana  imeanza mazoezi kujiandaa na mashindano wachezaji wa ndani (CHAN) yanayoandaliwa na Shirikisho la Vyama mpira barani Afrika (CAF)

Taifa stars imeingia kambini juzi kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Uganda utakaochezwa Uwanja wa Taifa  Julai 13, mwaka huu jijini Dar es Salaam na kurudiwa baada ya  wiki mbili jijini Kampala

Akizungumza na LENZI YA MICHEZO, Kocha Mkuu Kim Poulsen amesema kuwa wachezaji wote wameingia kambini na wote wamefanya mazoezi jambo ambalo linadhihirisha hakuna mwenye matatizo

“Wachezaji wote waliingia kambini tangu jana na leo wamefanya mazoezi wote pia wana ari jambo linalodhihirisha mchezo dhidi ya Uganda tutashinda” alisema Poulsen

Wachezaji wa Stars ni Juma Kaseja, Aggrey Morris, Aishi Manula, Ally Mustafa, Amri Kiemba, Athuman Idd, Frank Domayo, Haruni Chanongo, John Bocco, Juma Liuzio na Kelvin Yondani.

Wengine ni Khamis Mcha, Mrisho Ngasa, Mudathiri Yahya, Mwadini Ali, Mwinyi Kazimoto, Nadir Haroub, Salum Abubakar, Shomari Kapombe, Simon Msuva, David Luhende na Vincent Barnabas.


LENZI YA MICHEZO lilishuhudia wachezaji hao  wakiwa mazoezini Uwanja wa Karume jana asubuhi mazoezi ambayo yalianza saa 12:00 asubuhi na kumalizika saa 1:30 asubuhi pia jioni ilifanya mazoezi Uwanja wa Taifa






No comments:

Post a Comment