Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, July 15, 2013

TIMU YA TIGER YA MCHEZO WA ROOLBALL YAALIKWA KENYA KWENYE MAFUNZO LAKINI HATARINI KUTOSHIRIKI KUTOKANA NA UKATA

WACHEZAJI wa timu ya Tiger ya mchezo wa Rollball huenda wakashindwa kuhudhuria mafunzo kutokana ukata unaowakabili.

Timu hiyo imealikwa kushiriki mafunzo ya ukocha na urefa kwa mchezo huo yatakayofanyika  Nairobi nchini Kenya kuanzia Julai 26 hadi Julai 29, mwaka huu.

Akizungumza jijini, Sylvester Kasembe ambaye ni mmoja wa wachezaji wa timu hiyo alisema kuwa gharama za ushiriki kw mtu mmoja ni  Ksh. 2500 ambazo ni sawa Tsh. 50,000 huku gharama za nauli na malazi kwenda na kurudi ni Tsh. 200,000.

“Tunatakiwa kulipia ada ya ushiriki ambayo ni 50000 kwa mtu mmoja pia nauli na malazi kwa siku zote ni 200000 hivyo mtu mmoja anatakiwa kuwa na 250,000  hivyo watu 12 itakiwa 3,000,0000”, alisema Kasembe.

Kasembe amesema timu yao haina uwezo wa kuwasafirisha wachezaji kuhudhuria mafunzo hayo hivyo wanaomba wadau wawasaidie ili waweze kupata mafunzo hayo kwani ni sehemu ya maandalizi ya fainali za dunia zitakazofanyika Otoba nchini Nairobi.

Rollball  ni mchezo unaochezwa kwa mikono  kama mchezo wa mikono (handball) huku wachezaji wao wakiwa wamevaa viatu vya matairi na kwa sasa kiwanja cha mchezo huo kipo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Fainali za dunia za 2012 ambazo zilifanyika nchini India Tanzania ilifika hatua ya robo fainali.


No comments:

Post a Comment