Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, July 15, 2013

SAYARI WOMEN YAIPA KIPIGO CHA PAKA MWIZI VFL KELLINGHUSEN YA UJERUMANI

Mshambuliaji wa Sayari Fatuma Mustapha akiwatoka mabeki wa Vfl Kellinghusen ya Ujerumani wakati wa mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam

Mshambuliaji wa Sayari, Neema Kuga akiwatoka mabeki wa Kellinghusen



Mwamuzi Rahel Pallangyo akiwakagua wachezaji wa Vfl Kellinghusen

Sayari women

Vfl Kellinghusen

TIMU ya Sayari juzi iliifunga Vfl Kellinghusen ya Ujerumani mabao 9-1 kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Karume, Ilala, Dar es Salaam.

Sayari ambayo ilisheheni mamluki kibao ilikwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 3-0. Yaliyofungwa na Fatuma Mustapha dakika ya 14 na 20 na Neema Kuga aliyefunga dakika ya 37.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko lakini jahazi la Vfl Kellinghusen lilizidi kuzama baada ya kuongezwa mabao mengine kupitia kwa Esther Chabruma dakika ya 58.

Mabao mengine ya Sayari yalifungwa na Sophia Mwasikili alifunga mawili dakika za 61 na 86, Fatuma Mustapha tena alifunga bao dakika ya 75, Fatuma Bushiri dakika ya 85 msumari wa mwisho uligongewa na Sylvie Felix dakika ya 89.

Timu ya Vfl Kellinghusen ilipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Jule Mohr dakika ya 52 lililotokana na mpira wa adhabu baada ya beki wa Sayari Pulkeria Charaji kumfanyia madhambi mshambuliaji  wa Vfl Kellinghusen , Annika Ehlers nje ya eneo la hatari.

Akizungumza baada ya mchezo huo Katibu wa Chama cha Soka la Wanawake mkoa wa Dar es Salaam, (DWFA) Stephania Kabumba alisema anashukuru mchezo umechezwa vema na kuwapongeza Sayari kwa ushindi waliopata.


“Nashukuru mchezo umechezwa vema pia naipongeza Sayari kwa ushindi waliopata kwani wamedhirisha kuwa soka la wanawake linaweza kupererusha vema bendera ya nchi”, alisema Stephania.

No comments:

Post a Comment