MACHANGUDOA BRAZIL WAANZA KUJIFUNZA KIINGEREZA


BELO HORIZONTE, Brazil
MACHANGUDOA nchini Brazil, wameanza kujifunza Kingereza ili kutoa huduma motomto kwa maelfu ya mashabiki wa soka watakaoingia nchini humo kwa ajili ya kushuhudia michuano ya Kombe la Mabara, Juni mwaka huu na ile ya Kombe la Dunia mwakani.

Wasichana lukuki wanaofanya biashara ya kujiuza kwenye Jiji la Belo Horizonte, wamekuwa wakihudhuria madarasa ya kingereza kwa ajili ya kujifunza lugha hiyo.

Igor Fuchs amekuwa akifundisha machangudoa hao kingereza, lakini amesema masoma hayo yanaangalia zaidi lugha za kimapenzi ili wasichana hao wawe wajuzi wakati wakihudumia wateja kutoka mataifa mbalimbali.

Jiji hilo linamachangudoa zaidi ya 80,000, ambao wanasuburi kwa hamu mashindano hayo, lakini uongozi wa Jiji hilo unategemea jumla ya mashabiki 40,000 wataingia kwenye mji huo mwezi ujao, wakati zaidi ya mashabiki 140,000 watahudhuria fainali za Kombe la Dunia 2014.

Chama cha Machangudoa kwenye mji huo kimekuwa kikitoa elimu ya bure ya somo la Kingereza kwa wasichana hao wanaojiuza tangu Machi mwaka huu.

“Tunawafundisha jinsi ya kujieleza, lakini pia tunawafundisha kwa vitendo jinsi ya kutumia vifaa vya kufanyia mapenzi, iliwavijue kwa majina na jinsi ya kuvitumia au kuomba kutumia.” Alisema Fuchs, ambaye anafundisha lugha za Kihispaniola na Kifaransa pia.

No comments