RONALDO OLD TRAFFORD
MANCHESTER, England
JAVIER Hernandez ‘Chicharito’ atakuwa muhimu kwa mchakato wa
Manchester United kumrudisha Cristiano Ronaldo, Old Trafford.
Man United walikuwa wamepanga kutoa kiasi cha pauni milioni 65
pamoja na Luis Nani kwa ajili ya kumnasa Ronaldo mwisho wa msimu huu, lakini Real
Madrid wanamtaka Chicharito kwa pauni milioni 25 hata kama dili la usajili wa Ronaldo
litakwama.
Paris Saint-Germain tayari wameshaweka mezani kiasi cha pauni
milioni 80 kwa ajili ya Ronaldo — dau ambalo alisajili wa nalo alipotoka Man
United mwaka 2009.
Mabingwa wa Ligi Kuu England, Man United ni moja kati ya klabu
chache ambazo zinaweza kumsajili staa huyo wa Kireno mwenye miaka 28. Na juzi
klabu hiyo ilitangaza kuingiza zaidi ya pauni milioni 92 kwenye miezi mitatu ya
kwanza ya mwaka 2013.
Chicharito anaweza kuwa muhimu sana kwenye kufanikisha usajili
wa Ronaldo, ambaye mwenyewe anatamani sana kurudi Old Trafford, Japokuwa Sir
Alex Ferguson anataka kumbakisha Mmexico Man United.
Post a Comment