Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, April 9, 2013

REAL MADRID YAFUZU LICHA YA KUFUNGWA NA GALATASARAY MABAO 3-2 KWENYE MCHEZO WA UEFA CHAMPIONS LEAGUE


Makocha, Fatih Terim (kulia) na Jose Mourinho wakisalimiana kabla ya mtanange kuanza.
Ronaldo akishangilia pamoja na Higuan baada ya Ronaldo kuifungia timu yake Real Madrid Bao dakika ya 8 baada ya kupata pasi safi iliyowapita mabeki wa Galatasaray iliyotumwa na Higuan. Baada ya Galatasaray kufungwa goli moja wakaanza kuwaandama Real Madrid kwa mashabulizi ambayo pia hayakuzaa matunda mpaka kipindi cha kwanza kinaisha na huku wakitupa pasi za juu zisizokuwa na macho. 
Me again: Cristiano Ronaldo celebrates scoring his 10th Champions League goal of the season
Cristiano Ronaldoakishangilia baada ya kuifungulia bao timu yake usiku huu
Mimi tena......Cristiano Ronaldo akiwaongezea kibarua Gala...

Luka Modric akivutwa na Emmanuel Eboue wa Galatasaray ili asilete shida
Kipindi cha pili Galatasaray wakaja kivingine kwa muziki mwingine, dakika ya 57 mchezaji wa zamani wa Arsenal  Emmanuel Eboué akawapachikia bao kwa kuachia shuti kali ambalo lilikuwa hatari mpaka kipa Lopez wa Real Madrid hakutaka hata kulifata,
Galatasaray wakaongeza kasi na bidii wakapachika bao jingine baada ya wao Cristiano Ronaldo kuwakosa kosa. Dakika ya 71  mchezaji Wesley Sneijder akawaongezea Galatasaray bao jingine la pili, wakazidi kuwashangaza mashabiki jinsi walivyobadirika muda mfupi tu. Dakika ya 72 Mchezaji Didier Drogba akawashona bao la tatu la fasta la kisigino safi kwa kumchenga mchezaji wa Real Madrid na kipa Lopez kutoona ndani.Kama kawa....Drog!!

Mchezaji  Didier Drogba akishangilia baada ya kuifungia bao la tatu Galatasaray
Drogba akishangilia mara baada ya kufanya matusi ya 3-1 dhidi ya Real Madrid

Cristiano Ronaldo na Gonzalo Higuain...hoi...baada ya kushonwa bao la 3
Baadaye kwenye dakika za lala salama Cristiano Ronaldo aliwapachikia bao jingine la pili na kufanya 3-2
VIKOSI:
Galatasaray: Muslera, Eboue (Elmander 80), Zan, Kaya, Riera, Altintop (Amrabat 46), Felipe Melo, Inan, Sneijder, Bulut (Sarioglu 63), Drogba.
Subs Not Used: Iscan, Aydin Yilmaz, Balta, Kurtulus.
Booked: Sneijder, Eboue, Amrabat.
Goals: Eboue 57, Sneijder 71, Drogba 72.
Real Madrid: Diego Lopez, Essien (Arbeloa 31), Pepe, Varane, Fabio Coentrao, Khedira, Modric, Di Maria, Ozil (Albiol 81), Ronaldo, Higuain (Benzema 73).
Subs Not Used: Casillas, Marcelo, Callejon, Morata.
Sent Off: Arbeloa (90).
Booked: Arbeloa.
Goals: Ronaldo 8, 90.
Attendnace: 52,000
Referee: Stephane Lannoy (France)

No comments:

Post a Comment