Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, August 4, 2017

WACHEZAJI TAIFA STARS KUGAWANA MILIONI 22 ZA COSAFA



WACHEZAJI wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ wanatarajiwa kugawana sh. Milioni 22 ambazo ni zawadi ya mshindi wa tatu kutoka katika mashindano ya Baraza la Mpira wa Miguu kwa Nchi za Kusini mwa Afrika (Cosafa).
Akizungumza na mtandao huu, Ofisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Alfred Lucas alisema COSAFA imetoa zawadi ya dola 10,000 sawa na Sh. 22,000,000 kwa Taifa Stars baada ya kushinda na kushika nafasi ya tatu katika mashindano ya Castle Cosafa yaliyofanyika mwezi uliopita nchini Afrika Kusini.
“TFF imeamua fedha hizo zitolewe kwa wachezaji wote walioshiriki fainali hizo pamoja na benchi la ufundi pia Cosafa imetuma fedha za zawadi kwa wachezaji waliofanya vizuri katika kila mchezo,” alisema Lucas.
Wachezaji hao ni Shiza Kichuya aliyeibuka mchezaji bora wa mechi dhidi ya Malawi, Muzamiru Yassin aliyeibuka mchezaji bora wa mechi dhidi ya Angola, Erasto Nyoni aliyeibuka mchezaji bora dhidi ya Mauritius, Elius Maguri aliyeibuka mchezaji bora wa mechi dhidi ya Afrika Kusini.
Pia Lucas alisema kipa bora wa michuano hiyo ni Said Mohammed alizawadiwa moja kwa moja na Cosafa.
Tanzania ilishika nafasi ya tatu wakati Zimbabwe iliibuka bingwa na Zambia iliyshika nafasi ya pili.

No comments:

Post a Comment