Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, August 4, 2017

VODACOM YAGAWA VIFAA KWA TIMU ZA LIGI KUU MSIMU UJAO

KAMPUNI ya Vodacom Tanzania ambayo ni mdhamini mkuu wa ligi kuu imegawa vifaa vya michezo vyenye thamani ya zaidi ya sh 500 milioni kwa timu zote 16 kuelekea kuanza kwa msimu mpya wa ligi 2017/18.
Vifaa vilivyotolewa ni jezi, viatu vya mazoezi na mechi, soksi, vizuia ugoko, nguo za mazoezi, mabegi ya kusafiria, jezi za waamuzi na vibao vya kufanyia mabadiliko uwanjani ili timu hizo shiriki na bodi ya ligi ziendelee na maandalizi kabla ya kuanza kwa ligi Agosti 26.
Jezi za Yanga msimu huu wa 2017/18
Mkurugenzi wa Idara ya masoko na usambazaji wa Vodacom, Hisham Hendi amesema wamegawa vifaa vya michezo kwa timu zote shiriki kama mkataba unavyoelekeza.
“Tunayo furaha kugawa vifaa vya michezo kwa timu shiriki za ligi kwa mujibu wa mkataba tuliosaini, tuna imani ligi ya msimu huu itakuwa ngumu kutokana na maandalizi yanayofanywa na timu zote,” alisema Hendi.
Jezi za Simba msimu wa 2017/18
Kwa upande wake Mkurugenzi wa bodi ya ligi Boniface Wambura amezitaka klabu kutumia nembo ya mdhamini mkuu kama ilivyoelekezwa ili kutokiuka masharti na kuadhibiwa.
“Nataka nizikumbushe klabu kuhakikisha zinafuata makubaliano ya mkataba kwa kutumia vifaa vilivyotolewa,” alisema Wambura.

No comments:

Post a Comment