Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, March 4, 2017

SIMBA YATOKA SARE YA 2-2 KWA MBEYA CITY






VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba leo wameshindwa kuondoka na pointi tatu baada ya kulazimishwa sare kufungana mabao 2-2 na Mbeya City `Koma Kumwanyakatika mchezo uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Wenyeji Simba walionekana kuzidiwa katika kipindi cha kwanza baada ya Mbeya City kupata bao la kuongoza katika dakika ya 37 lililofungwa na Ditram Nchimbi kufuatia pasi ya Kenny Ally.
Simba walipata bao la kusawazisha katika dakika ya 65 mfungaji akiwa ni Ibrahim Ajibu, baada ya kupiga mpira wa adhabu uliojaa wavuni moja kwa moja.
Mbeya City waliongoza tena baada ya kupata bao la pili katika dakika ya 78 lililofungwa na Kenny Ally baada ya kupata pasi kutoka kwa Nchimbi.
Dakika nne kabla ya mchezo kumalizika, Simba walipata bao la kusawazisha lililofungwa kwa penalti na Kichuya baada ya Mohamed Hussein kuangushwakatika eneo la hatari.
Simba ilifanya shambulio la nguvu katika dakika ya 12 na Kichuya alikosa bao la wazi baada ya kichwa alichopiga kudakwa na kipa wa Mbeya City, Own Chaima.
Ajibu nusufa afunge katika dakika ya 40, lakini lilimbabatiza kipa wa Mbeya City na kutoka nje.
Timu hizo zilikwenda mapumziko Mbeya City ikiwa mbele kwa bao 1-0.
Kwa matokeo hayo, Simba imefikisha pointi 55 na kuwa mbele kwa pointi tatu dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wenye pointi 52, ambao leo wanacheza na Mtibwa Sugar mjini Morogoro.
Simba wiki iliyopita iliifunga Yanga mabao 2-1 na kutarajiwa kuonesha makali zaidi katika mchezo huo wa jana dhidi ya Mbeya City, ambayo mwendo wake sio mzuri katika ligi hiyo.
Vikosi vilikuwa, Simba:
Daniel Agyei, Hamas Juma, Mohamed Hussein, Abdi banda, James Kotei, Jonas Mkude, Mzamiru Yasini, Ibrahim Ajibu, Laudit Mavugo, Said Ndemla na Shiza Kichuya.
Mbeya City:
Own Chaina, John Kabanda, Majaliwa Shabani, Tumba Sued, Rajabu Zahiri, Kenny Ally, Sankani Mkandawile, Raphael Daud, Ditram Nchimbi, Mrisho Ngasa na Rafael Brayson.

No comments:

Post a Comment