Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 18, 2017

YANGA YALAZIMISHWA SARE, KUKUTANA NA ZESCO SASA






WAWAKILISHI wa Tanzania katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika Yanga, leo walishindwa kutoka na karamu ya mabao baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Ngaya na Comoro kwenye Uwanja wa Taifa.
Mashabiki wa soka nchini walitarajia ushindi wa mabao mengi kutoka kwa Yanga hasa ukizingatia kuwa timu hiyo ilipata mabao 5-1 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Moroni wikiendi iliyopita.
Yanga sasa imesonga mbele kwa ushindi wa jumla ya mabao 6-2 na kuisubiri ama Zanaco ya Zambia au APR ya Rwanda, ambazo nazo zilikuwa zikicheza jana Kigali.
Katika mchezo wa jana, Ngaya ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za Yanga baada ya kufunga bao la kuongoza katika dakika ya 19 lililofungwa na Zamir Mohamed baada ya shuti kumbabatiza Bossou na kumpoteza kipa Deogratius Munish na kujaa wavuni.
Yanga walisawazisha dakika mbili kabla ya mapumziko kwa bao la Hajj Mwinyi aliyepiga shuti kali la mbali lililokwenda moja kwa moja wavuni.
Awali, dakika nne tangu kuanza kwa mchezo, Yanga walikosa bao baada ya Emmanuel Martine kushindwa kuunganisha wavuni mpira wa krosi uliopigwa na Juma Abdul.
Martine alikosa bao tena dakika nane baadae kufutia krosi ya Simon Msuva.
Ngoya walifanya shambulio la nguvu katika dakika ya tisa na nusura wafunge bao, lakini Rakotoariamanana Falinirino alishindwa kufunga licha ya kuwa yeye na kipa na kupiga nje.
Kikosi Yanga
Deogratius Munish, Juma Abdul, Mwinyi Haji, Kelvin Yondan, Vecent Bossou, Justine Zullu, Simon Msuva, Thaban Kamusoko, Deus Kaseke, Obrey Chirwa na Emmanuel Marrine.


No comments:

Post a Comment