Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 11, 2017

SIMBA YAREJEA KILELENI






SIMBA imeiengua Yanga kileleni katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifunga Tanzania Prisons kwa mabao 3-0 na kufikisha pointi 51.
Kwa ushindi huo, Simba wameiacha Yanga na pointi zake 49 baada ya mabingwa hao watetezi jana kutoshuka dimbani baada ya kuwa na mechi ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika dhidi ya timu ya Comoro.
Simba huenda ikakalia kiti hicho kwa muda kama Yanga watashinda mchezo wao dhidi ya watani zao hao wa jadi katika mchezo utakaofanyika Februari 25 kwenye Uwanja wa Taifa.
Yanga inarudiana na Wacomoro Jumamosi katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Katika mchezo huo wa jana, Simba waliandika bao la kwanza katika dakika ya 18 lililofungwa na Juma Luizio baada ya kupigwa kona ya `nje kabla ya mpira kumkuta mfungaji aliyeujanza wavuni.
Dakika 10 baadae Simba waliandika bao la pili kupitia kwa Ibrahim Ajibu akiunganisha wavuni krosi ya Laudit Mafugo.
Wekundu hao wa Msimbazi waliandika bao la tatu lililofungwa na Laudit Mavugo kwa kichwa akiunganisha krosi ya Ajibu.

Simba: Daniel Agyei,Method Mwanjale/Mwinyi Kazimoto, Javier Bukungu, Mohamef Hussein, Novalty Lufunga, Said Ndemla, James Kotei, Mzamiru Yassin, Ibrahim Ajibu/Pastor Athanas, Laudit Mavugo na Juma Luizio/Shiza Kichuya.
Prisons: Laurian Mpalile, Aron kalambo, Salum Kimenya, James Mwasote, Nurdin Chona, Jumanne Elifadhili, Lambart Sabiyanka, Kazungu Nchinjayi/Kassim Hamis, Victor Hangaya, Mohamed Samata na Benjamin Asukile/Meshaki Selemani.




No comments:

Post a Comment