Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, February 16, 2017

MAVUGO AIPELEKA SIMBA ROBO FAINALI KOMBE LA FA






NYOTA ya mshambuliaji wa Simba, Mrundi Laudit Mavugo imezidi kung’ara baada ya leo kuifungia timu yake bao pekee na kuipeleka robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho (FA) kwa kuifunga African Lyon bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Hiyo ni mechi ya tatu mfululizo kwa mshambuliaji huyo kufunga kwenye michuano yote inayoshiriki Simba, baada ya kufunga bao moja katika kila mechi dhidi ya Majimaji na Prisons.
Iliichukua dakika 58 kwa Mavugo kufunga bao hilo baada ya kuunganisha pasi nzuri ya Saidi Ndemla kabla ya kuujaza mpira nyavuni.
Simba ilicheza vizuri katika mechi hiyo na ilianza kwa kulishambulia lango la wapinzani wao tangu mwanzo wa mchezo.
Dakika ya 16, Mavugo alipoteza nafasi ya kufunga kabla ya Juma Luizio kukosa nafasi nyingine baada ya shuti lake kupanguliwa na kipa wa Lyon  Rostand Youthe.
Dakika ya 32, Ibrahim Ajibu alipoteza nafasi nyingine ya kufunga baada ya shuti lake kupaa juu ya lango akiwa yeye na kipa.
Katika kipindi cha pili,Simba ilifanya mabadiliko kwa kuwatoa Luizio na Ndemla na nafasi zao kuchukuliwa na Shiza Kichuya na Mohamed ‘Mo’ Ibrahim.
Hata baada ya mabadiliko hayo, Simba haikumudu kuongeza bao kwani Lyon walionekana wakicheza kwa tahadhari kubwa kuepuka kufungwa mabao mengi.
Simba na Lyon zimekutana kwa mara ya pili msimu huu, mara ya kwanza ilikuwa kwenye mechi ya Ligi Kuu ambapo Simba ilifungwa bao 1-0 na Lyon kwenye uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.
Simba: Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Abdi Banda, Jonas Mkude, Novaty Lufunga, James Kotei, Said Ndemla/Mohammed ‘Mo’ Ibrahim dk70, Laudit Mavugo/Pastory Athanas dk85, Ibrahim Ajibu na Juma Luizio/Shiza Kichuya dk59.
African Lyon: Rostand Youthe, Miraji Adam, Baraka Jaffary, Omary Salum, Hamad Waziri, Hassan Isihaka, Peter Mwalyanzi, Hamad Manzi/Awadh Juma dk49, Rehani Kibingu, Venance Joseph na Omary Daga/Fred Cosmas dk72.

No comments:

Post a Comment