Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, August 16, 2016

WANACHAMA YANGA WAMPIGIA MAGOTI MANJI



WANACHAMA wa klabu ya Yanga Kanda ya Dar es Salaam wamempigia magoti na kumsihi abadili maamuzi yake Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji,  kubadili msimamo wake wa kutoikodi timu hiyo
Wanachama hao wamemuomba Manji asibadili msimamo wake katika kikao cha dharura kilichoketi leo kwenye makao Makuu ya timu hiyo yaliyopo jijini Dar es Salaam.
Pia wanachama hao wamekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa timu hiyo kuzungumza na vyombo vya habari pasipo kupata ridhaa ya chama.
Mwenyekiti wa Matawi ya Yanga Kanda ya Dar es Salaam, Robert Lyungu Kasera amemtaka katibu wa timu hiyo Taifa kumfuta uanachama Katibu wa Baraza la wazee la Yanga Taifa, Ibrahim Akilimali kwa madai kuwa kiongozi huyo anashirikiana na timu pinzani kukwamisha mpango wa Manji kuikodi timu.
“Akilimali anashirikiana na Simba kuiharibu Yanga hatufahi, haiwezekani aongelee masuala ya Yanga pasipo ridhaa ya uongozi wa klabu mfikishe taarifa hii kwa usahihi bila kumungunya na kikao hiki kinalaani kitendo alichofanya,” amesema Lyunga.
Zameda Mageka mwanachama wa Yanga tawi la Wakali Temboni ameitaka Yanga kumsimamisha Akilimali na kumteua Katibu mwengine kushika wadhifa wake.
Taarifa zisizo rasmi zinadai kuwa uamuzi wa Manji kutaka kubwaga manyanga unatokana na kauli za matusi na kejeli kutoka kwa baadhi ya viongozi wa ndani ya Yanga na serikalini.



No comments:

Post a Comment