Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, August 16, 2016

WAJUMBE WATATU WALIOVULIWA UANACHAMA YANGA WAKATA RUFAA TFF



WAJUMBE watatu wa  Yanga ambao walivuliwa uanachama wamepeleka barua yao kupinga hatua hiyo katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF).
Akizungumza na wandishi wa habari afisa habari wa TFF, Alfred Lucas amesema barua hiyo iliwasilishwa katika shirikisho hilo Agosti 12, 2016.
“Wanachama  Ayoub Nyenzi, Hashim Abdallah na Mkemi ni wajumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga ambao walivuliwa uanachama Agosti 6, mwaka huu walileta barua ya malalamiko TFF, ” amesema Lucas.
Ameongeza kuwa “nathibitisha kuwa malalamiko yao yamepokelewa ambayo yanalenga kutaka haki itendeke.”
Amesema barua hiyo inasema kuwa uongozi wa Yanga ulikiuka taratibu na katiba ya klabu hiyo ilipowafuta uanachama.
“TFF imeyapokea malalamiko hayo na yatapelekwa katika kamati husika pindi yatakapofanyiwa maamuzi tutawajulisha wadau wa mpira wa miguu nchini,” amesema.

No comments:

Post a Comment