Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, August 16, 2016

ATN KUONESHA LIVE YANGA NA AZAM FC KESHO




Mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Azam Fc na Yanga Fc inayotarajiwa kuchezwa kesho katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam inatawanufaisha wanafunzi wa kwani sehemu ya mapato itatumika kununulia madawati 200.
Akizungumza na wandishi wa habari leo Afisa habari wa shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania  (TFF)  Alfred Lucas amesema kuwa mchezo huo utaoneshwa na Ting  kuptia chanel ya ATN na sehemu ya mapato yapelekwa kwa katibu mkuu wa bunge, Dr. Kashilila kwani wao wanaisaidia serikali kuchangia madawati.
“Ting wamepata haki ya kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mechi ya kesho kama ambavyo huwa wanarusha matangazo ya mechi ya ligi za Uingereza “ amesema Alfred
Naye Mkurugenzi wa Michezo kutoka Ting, Dennis Msemo ameomba wadau kuhudhuria mchezo huo wa ngao ya jamii
“Sisi kupitia king’amuzi cha Ting tutaonesha mchezo kwenye chaneli ya ATN tunawaomba wadau wote wa Michezo na Vyombo vya Habari kujumuika nasi pale uwanja wa Taifa kuanzia saa kumi jioni, tunahitaji ushirikiano wetu wa hali na mali. Sisi ajenda yetu kubwa ni michezo, na michezo kwetu ni utamaduni na hii ndio kauli mbiu yetu” Amesema Dennis.

No comments:

Post a Comment