Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, August 13, 2016

SWANSEA CITY WAVUNJA BENKI NA KUWEKA REKODI YA KUMSAINI BORJA BASTON WA ATLETICO MADRID

Swansea City wamevunja Rekodi ya Klabu yao kwa kumsaini Straika kutoka Spain Borja Baston kutoka Atletico Madrid kwa Pauni Milioni 15.
Borja, mwenye Miaka 23, alifunga Bao 18 kwenye La Liga Msimu uliopita akiwa kwa Mkopo na Eibar.
Dau la kumnunua Borja limiezidi lile la Mwaka 2013 Swansea walipomnunua Wilfried Bony.
Borja amekuja wakati muafaka baada ya Swansea kuondokewa na Mafowadi Andre Ayew alieenda West Ham, Alberto Paloschi, Eder na Bafetimbi Gomis.
Hivi Juzi Swansea pia walimchukua Mchezaji mwingine wa Spain Fernando Llorente na hadi sasa Kocha Mpya Francesco Guidolin ameshasaini Wachezaji Watano na wengine ni Beki wa Holland Mike van der Hoorn, Winga wa Holland Leroy Fer na Kipa wa Australian Mark Birighitti.
 

No comments:

Post a Comment