Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, August 9, 2016

MAVUGO AKIRI KAZI IPO KUPATA NAMBA MSIMBAZI




MSHAMBULIAJI wa Simba, Laudit Mavugo  amesema lazima aongoze bidii ili kujihakikishia kupata namba kwenye kikosi cha kwanza.
Akizungumza na gazeti hili baada ya kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya AFC Leopard ya Kenya,  Mavugo kuanzia aanze mazoezi na mchezo aliocheza amegundua upinzani ndani ya kikosi chao.
"Nimekuja kucheza na ndiyo kazi yangu, lazima niongeze jitihada ili kuhalikisha napata namba, sijaifahamu Simba kiundani ila kwa haraka haraka nimeona ni timu yenye ushindani",  alisema Mavugo
Kwenye kikosi cha Simba kinachonolewa na Joseph Omog, Mavugo atakuwa na kazi ya kuwania namba na  Ame Ally, Ibrahim Ajibu, Danny Lyanga na Fredric Blagnon ambaye ni raia wa Ivory Coast. 
Mavugo amesaini miaka miwili Simba akitokea Vital O ya Burundi na amesisitiza kuwa amekuja Simba kulipa deni kwani mwaka jana  alichukua pesa ya usajili na hawakumshtaki  kudai haki yao baada kushindwa kutua Simba.
Katika kusheherekea tamasha la Simba lililofanyika juzi, Mavugo alisherehesha furaha ya wana Msimbazi baada ya kufunga bao la nne kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Taifa.



No comments:

Post a Comment