Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, August 6, 2016

MAKOCHA 26 WA MAKIPA WAFUZU KOZI YA JUU









KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) Selestine Mwesigwa amewaasa makocha wa magolikipa kuitumia vema taaluma waliyoipata.
Mwesigwa alitoa rai hiyo wakati akifunga kozi ya juu ya makocha wa magolikipa iliyokuwa inaendeshwa na mkufunzi wa Fifa, Alejandro Heredia.
“Mpira ni golikipa hivyo taaluma yenu ni muhimu sana kwa mustakabali wa soka la Tanzania hivyo mkawe chachu ya soka mkishirikiana ninyi kwa ninyi”, alisema Mwesigwa.
Pia Mwesigwa alisema kama mwenzenu atahitaji msaada msaidiane na siyo kukaa kimya wakati timu yake ikifanya vibaya.
Naye Mkufunzi Heredia aliwashukuru makocha hao kwa ushirikiano waliompa kwani wamefanya kazi yake kuwa rahisi na anaamini watakuwa makocha bora wa makipa.
Kozi hiyo ya siku saba ilikuwa na washiriki 26 toka kwenye timu za ligi kuu Tanzania Bara na timu za Taifa.

No comments:

Post a Comment