Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 27, 2016

YANGA YAWAPA RAHA MASHABIKI TAIFA LEO BAADA YA KUFUZU HATUA YA PILI KLABU BINGWA








YANGA imeleta heshima kwa Watanzania baada ya leo kuifunga Cercle de Joachim ya Mauritius katika mchezo wa maruadiano Ligi ya Mabingwa Afrika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kutokana na matokeo hayo Yanga imefuzu hatua inayofuata kwa jumla ya mabao 3-0, baada ya mchezo wa kwanza uliofanyika nchini Mauritius wiki mbili zilizopita Yanga kushinda bao 1-0.
Ilikuwa furaha kwa mashabiki wa Yanga walioingia jana kifua mbele ikiwa ni wiki moja baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya watani zao Simba katika Ligi Kuu Tanzania Bara.
Hata hivyo Yanga licha ya ushindi huo, itabidi ijilaumu kutokana na kukosa nafasi nyingi za wazi, ambazo zingewawezesha kupata ushindi mnono.
Lakini washambuliaji wake wakiongozwa na Amis Tambwe, Simon Msuva, Malimi Busungu na Paul Nonga kwa nyakati tofauti walishindwa kulenga lango la wapinzani wao.
Washambuliaji hao kila walipokaribia lango la Yanga, ama walipiga michomo dhaifu iliyodakwa na kipa au walipiga nje ya lango.
Yanga ilianza kupata bao la mapema dakika ya tatu mfugaji akiwa Amiss Tambwe kutokana na krosi ya Simon Msuva.
Bao hilo liliwapa matumaini mashabiki wa Yanga kuona ushindi mnono, lakini kadri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo matumaini hayo yalipokuwa yakififia.
Wageni walijitahidi kupanga mashambulizi dakika za mwanzo kipindi cha pili, lakini walijikuta wakipachikwa bao la pili dakika ya 56 mfungaji akiwa kiungo Thabani Kamusoko kwa shuti lilitokana na mpira wa adhabu wa Juma Abdul.
Yanga itakumbana na mshindi wa mchezo kati ya APR ya Rwanda na Mbabane Swallows ya Swaziland.

No comments:

Post a Comment