Chelsea kuachana na Terry mwishoni kwa msimu huu
Nahodha wa Chelsea, John Terry
anatarajiwa kuachana na klabu yake ya Chelsea baada ya timu hiyo
kuonyesha nia ya kutokuhitaji kuongeza mkataba na mchezaji uyo.
Terry
aliyejiungana Chelsea akiwa na miaka 14 aliweka wazi mipango ya klabu
yake kuachana na nae na kueleza kuwa anapendelea kusalia katika klabu
hiyo lakini uongozi unaonekana kutokuhitaji kuendelea nae.
“Napenda kuendelea kubaki hapa lakini uongzi wa klabu unaonekana kuwa tofauti,” alisema Terry.
Hata
hivyo mmoja wa wazungumzaji wa klabu hiyo alikaririwa Jumapili akisema
kuwa Terry bado hajapewa mkataba mpya na bado uongozi haujaamua hatama
ya mchezaji huyo,
Terry
mpaka sasa ameshaichezea Chelsea michezo 696 na amefanikiwa kushinda
makombe manne ya Ligi Kuu ya Uingereza, makombe ya FA Cup mara tano na
kombe moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya.
No comments:
Post a Comment