Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, February 12, 2016

SIMBA KUONGOZA LIGI KWA MUDA KESHO?






SIMBA na Azam FC na kesho na jumapili zina nafasi kubwa ya kuiengua Yanga kileleni endapo zitashinda mechi zao za Ligi Kuu Tanzania Bara zitakazopigwa kwenye viwanja tofauti.
Yanga inayoongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 43 haitashuka dimbani wikiendi hii katika mchezo wa ligi hiyo kwani inacheza na Cercle De Joachim Mauritius katika mchezo wa awali wa Ligi ya Mabingwa wa Afrika.
Simba na Azam FC wako katika nafasi ya pili na tatu na wamefunga kwa pointi, ambapo kila moja ina pointi 42 na kama zitashinda zitafikisha 45 na kuiondoa Yanga kileleni.
Simba ambao tangu waanze kufundishwa na Mganda Jackson Mayanja wameshinda mechi zao zote, leo watakuwa wageni wa Stand United katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Stand United wako katika nafasi ya tano na watataka kuizuia Simba na kudhihirisha makali yao, hivyo pambano hilo linatarajiwa kuwa lenye ushindani wa hali ya juu kutoka kwa timu hizo.
Wenzao Azam FC nao watakuwa ugenini wakicheza na Coastal Union ya Tanga katika mchezo utakaofanyika kesho kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
Azam FC kabla ya mchezo wa huo wako nyuma kwa mechi mbili, hivyo kama itashinda zote itafikisha pointi 48, hivyo ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri ukilinganisha na Simba na Yanga.
Katika mchezo mwingine; Mgambo JKT                 itacheza na kaka zao wa African Sports kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Mbeya City watakuwa wageni wa Toto Africans, Ndanda FC        dhidi ya Majimaji.
JKT Ruvu wataikaribisha Kagera Sugar wakati Mwadui ya Shinyanga itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons.

No comments:

Post a Comment