Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, December 12, 2015

SIMBA NA YANGA ZATOKA SARE LEO






VINARA wa Ligi Kuu Bara, Azam leo wamelazimishwa sare ya mabao 2-2 na Simba katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Wakati Azam ikipata matokeo hayo, mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Yanga nao walishindwa kuibuka na ushindi kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga na kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya Mgambo.
Matokeo hayo yanafanya timu hizo kugawana pointi moja moja humu Azam ikiendelea kukaa kileleni baada ya kufikisha pointi 26, Yanga ikishika nafasi ya pili kwa kufikisha pointi 24 na Simba ikiwa na pointi 22 katika nafasi yake ya nne.
 Kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam, mpaka mapumziko timu zilikuwa sare ya bao 1-1, Azam ikianza kupata bao la kuongoza lililofungwa na John Bocco  sekunde ya 58 na Ibrahim Hajib akiisawazishia Simba katika dakika ya 24.
Kuingia kwa bao hilo kuliichanganya Azam ambapo waliruhusu mashambulizi mfululizo langoni mwao na kama si uimara wa kipa Aishi Manula, Simba ingepata mabao mengi.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikicheza kwa tahadhari na Hajib akaiongezea Simba bao la pili katika dakika ya 68 kwa shuti kali.
Dakika chache baadae Bocco aliisawazishia Azam bao hilo na kufanya mchezo uzidi kuwa mgumu huku kila upande ukisaka ushindi katika dakika zilizosalia bila mafanikio.
Kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga, timu zote zilishambuliana kwa zamu na mpira ulikuwa wenye rafu nyingi kwa wachezaji wa pande zote.
Katika mechi nyingine Majimaji ikiwa nyumbani Songea imelala kwa mabao 4-0 kutoka kwa Toto Africans huku Mbeya City ikitoka sare ya mabao 2-2 na Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya.
Kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora Kagera Sugar ilitoka sare ya bao 1-1 na Ndanda huku Stand United ikiambulia kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Mwadui.

No comments:

Post a Comment