MENEJA
wa Man City Maneul Pellegrini anaamini kipigo chao kutoka kwa Arsenal
Jumatatu iliyopita cha 2-1 huko Emirates hakitaathiri kampeni yao ya
kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Msimu huu.
Kipigo hicho kimewaacha Man
City wakiwa Nafasi ya 3 Pointi 4 nyuma ya Arsenal ambao wako Nafasi ya
Pili wakiwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Leicester City. Leo Man City wapo kwao Etihad kucheza na Sunderland ambao kawaida huivimbia City wakati Leicester na Arsenal zote ziko Ugenini kwa Arsenal kucheza huko Saint Mary na Southampton na Leicester kuwa Anfield kuivaa Liverpool.
Ikiwa Leicester watatetereka na Arsenal kushinda, basi Arsenal watatwaa uongozi hii Leo.
![](http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/media/motion/ESPNi/2015/1223/int_151223_Allardyce_pressr/int_151223_Allardyce_pressr.jpg&w=738&site=espnfc)
Lakini Pellegrini anaamini City, iliyotwaa Ubingwa Mwaka 2012 na 2014, inaweza kushinda Mechi yake ya Leo na ya Jumanne Ugenini na Leicester.
Pellegrini ameeleza: “Tupo Nafasi ya 3, Pointi 4 nyuma ya Arsenal na Pointi 6 nyuma ya Leicester. Ni muhimu kushinda Mechi zetu hizi 2 za sasa tumalize Raundi ya kwanza ya Ligi tupo juu. Kitu muhimu ni kuimaliza Januari tuko juu, kisha tujaribu na kutwaa Ubingwa!”
![](http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/media/motion/ESPNi/2015/1222/int_151222_INET_FC_PELLEGRINI_DISC/int_151222_INET_FC_PELLEGRINI_DISC.jpg&w=738&site=espnfc)
Habari njema kwa Pellegrini ni kurejea Uwanjani kwa Kepteni wake Vincent Kompany ambae alikuwa Majeruhi na Msimu huu katika Mechi 8 alizocheza City haijafungwa na ilishinda Mechi 6 na kufungwa Bao 1 tu wakati kipigo cha Arsenal ni Mechi yao ya 5 kati ya 9 ambazo walifungwa bila Kompany.
![](http://gamingtips.org.uk/wp-content/uploads/2014/12/Barclays-Premier-League-logo-660x330.jpg)
RATIBA MECHI ZA LEO HII JUMAMOSI BOXING DAY!
Jumamosi Desemba 26
15:45 Stoke v Man United
18:00 Aston Villa v West Ham
18:00 Bournemouth v Crystal Palace
18:00 Chelsea v Watford
18:00 Liverpool v Leicester
18:00 Man City v Sunderland
18:00 Swansea v West Brom
18:00 Tottenham v Norwich
20:30 Newcastle v Everton
22:45 Southampton v Arsenal
No comments:
Post a Comment