Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, December 26, 2015

NAPE NNAUYE AWATAKA WATANZANIA KUMUOMBEA RAIS DK JOHN POMBE MAGUFULI, KWANI KAZI YA KUTUMBUA MAJIPU NI NGUMU NA INA VIKWAZO VINGI

1
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Ndugu Nape Nnauye  aliyekuwa mgeni rasmi akimuwakilisha Makamu wa Rais Mh. Mama Samia Suluhu Hassan akizindua rasmi albam mbili za kwaya ya Wakorintho wa Pili kwenye tamasha la Krismas lililofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee leo, ambapo mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika ya Kusini Rebecca Malope amefanya onesho kubwa lililovuta hisia za mashabiki wengi waliohudhuria katika tamasha hili akishirikiana na waimbaji mbalimbali wa hapa nyu mbani na nchi jirani ya Kenya.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Nape Nnauye amewaomba watanzania kuzidi kumuombea Rais Dk . John Pombe Magufuli kwa kazi ya kutumbua majipu ambayo amekwishaianza kwani kazi hiyo ni ngumu na ina vikwazo vingi, lakini pia amewataka watanzania na waumini wa madhehebu mbalimbali kuwaombea wasaidizi wake ili waweze kuwa bega kwa bega na Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli ili kutekeleza kazi hii kwa ufanisi na kisha watanzania wafaidi matunda na rasilimali zao wenyewe.
Waimbaji kutoka Kenya walikuwa ni Faustine Munishi na Sara K na Solomon Mukubwa  kutoka jiji la Nairobi huku  waimbaji wa hapa nyumbani wakiwa ni  Rose Muhandom Upendo Nkone, Christine Shusho, Edson Mwasabwite, Joshua Mlelwa na wengine wengi, Tamasha hilo pia lilikuwa na lengo la kumshukuru mungu kwa nchi yetu ya Tanzania kufanya uchaguzi kwa amani, Kulia ni Akex Msama Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion ambayo ndiyo imeandaa tamasha hilo.(PICHA NA JOHN BUKUKU-  FULLSHANGWEBLOG-DAR ES SALAAM)
2
Akex Msama Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion ambayo ndiyo imeandaa tamasha hilo. akimkaribisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Ndugu Nape Nnauye ili kuzungumza na wananchi katika tamasha hilo kushoto ni Mbunge Martha Mlata na MC Mwakipesile mshereheshaji wa Tamasha hilo.
3
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Ndugu Nape Nnauye akiwahutubia wananchi na mashabiki waliohudhuria katika tamasha hilo katikati ni Akex Msama Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion ambayo ndiyo imeandaa tamasha hilo na kushoto ni MC Mwakipesile.
4
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Ndugu Nape Nnauye akiimba moja ya mapambio na kuitikiwa na mashabiki wa nyimbo za injili waliohudhuria katika tamasha hilo.
5
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Ndugu Nape Nnauye pamoja na maaskofu na viongozi mbalimbali wakishiriki katika sala maalum ya maombi iliyofanyika katika tamasha hilo,
6
Wamumini na mashabiki mbalimbali wa muziki wa injili wakishiriki katika maombi maalum ya kumshukuru mungu yaliyofanyika kwenye tamasha hilo.
7
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Ndugu Nape Nnauye na mkewe Mrs Rhobi Nape Nnauye wakicheza pamoja na mwimbaji Upendo Nkone kutoka kulia ni Mbunge Martha Mlata na Alex Msama wakishiriki kucheza.
8 9
Mwimbaji Rebecca Malope akiimba katika tamasha hilo.
10
Waimbaji wa mwimbaji Rebecca Malope akiimba  katika tamasha hilo.
11
Mwimbaji Rebecca Malope akiimba kwa hisia huku meza kuu pamoja na mashabiki wake wakiwa wamesimama.
14
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Ndugu Nape Nnauye na mkewe Mrs Rhobi Nape Nnauye pamoja na maaskofu mbalimbali wakiwa wamesimama wakati  mwimbaji Rebecca Malope akifanya vitu vyake katika  tamasha hilo.
15
Mwimbaji Christine Shusho na Mbunge Martha Mlata wakiimba pamoja wakati wa Tamasha hilo.
16
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Ndugu Nape Nnauye na mkewe Mrs Rhobi Nape Nnauye,Alex Msama na Mkewe na baadhi ya wabunge kulia ni Martha Mlata na kushoto ni Mary Majelwa wakiwa katika picha ya pamoja.
17
Mwimbaji Faustine Munishi kutoka nchini Kenya akiiimba katika tamasha hilo.
18
Wanakwaya wa Wakorintho wa pili wakiimba wimbo wao mara baada ya kuzinduliwa kwa albam zao katika tamasha hilo.
19
Mwimbajo kutoka nchini Kenya Solomon Mukubwa akiimba na mwimbaji mwenzake kutoka kushoto  Sara K. huku mbunge  Martha Mlata akishiriki kuimba nao.
20
Mwimbaji Joshua Mlelwa naye amefanya mambo makubwa jukwaani katika tamasha hilo.
21
Mwimbaji Rose Muhando pamoja na waimbaji wake wakifanya vuti vyao jukwaani.

No comments:

Post a Comment