Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, August 5, 2015

TFF YAFUNGA NDOA TENA NA VODACOM KWA MIAKA MITATU



SHIRIKISHO la Mpira la Soka Tanzania (TFF) limesaini mkataba mpya wa miaka mitatu wa udhamini wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.
Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa amethibitisha kusainiwa kwa mkataba huo na kusema hawakufanya sherehe za kutia saini mkataba huo kutokana na  mashindano ya Kagame yaliyokuwa yanaendelea nchini kwani TFF ndio iliyokuwa ikiyasimamia kama shirikisho la soka mwenyeji.
“Wanasema katika ajira, unaposikia nafasi haijatangazwa na hajatangazwa mtu mpya basi kuna maendeleo na mara nyingi mkataba unaoendelea uliokuwepo ukisainiwa tena ‘renewal contract’ haivuti masikioni kama unapoongelea mkataba ambao watu wameingia udhamini mpya”, amesema Mwesigwa.
Pia Mwesigwa aliweka wazi kuwa mdhamini wa ligi msimu unaokuja ni Vodacom ambao walikuwepo msimu uliopita kwani kila kitu kimeshawekwa sawa ila kwa maana ya sherehe ndio bado haijafanyika kwasababu kulikuwa na mambo mengi hapa katikati ikiwa ni pamoja na mashindano ya Kagame.
Pamoja na kukiri kuwa TFF imeshakubaliana na Vodacom kuendelea kwa miaka mitatu ijayo lakini hakuweka wazi jinsi mkataba huo ulivyoboreshwa kwa madai hadi sherehe za kutiana saini zitakapofanyika.
“Mkataba ni miaka mitatu, kutakuwa na maongezeko ukizingatia kuna timu zimeongezeka lakini nadhani hata kile kinachokwenda kwenye vilabu kitaongezeka kwa kiasi fulani yako masuala mengi siwezi kuzungumza kwa undani kwa sasa hivi pia kwa upande wa kwetu tulikuwa  na mambo ambayo tuliyaona hayapo sawa hivyo kulikuwa na muda mwingi wa kutosha kujadili karibu miezi nane iliyopita kwa hiyo vitu vingi vimeangaliwa”, alisema Mwesigwa.
Vodacom wamekuwa wakidhamini ligi kuu lakini kumekuwepo malalamiko mengi kwa klabu kuwa kiasi wanachotoa hakitoshelezi ukizingatia baadhi ya timu hazina mfadhili

No comments:

Post a Comment