Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, May 24, 2015

Washindi wa tuzo za Watu 2015, hawa hapa


TIIPichani wakati wa tuzo za watu ilivyokuwa baada ya washindi kukabidhiwa  tuzo zao..

Hatimaye usiku wa Mei 22 Tanzania iliandika historia nyingine kwa kushuhudia utoaji wa tuzo maalum zijulikanazo kama TUZO ZA WATU 2015, zilizofanyika jijini Dar es Salaam.
Washindi hao  ni katika vipengele 13 vya mwaka huu. Majina hayo ya washindi yaliingia baada ya kuvuka michujo miwili migumu. Ni kura za mashabiki peke yake ndio ziliwaingiza kwenye fainali hiyo na mshindi aliweza kupatikana kwa kura za wananchi , kama alivyonukuliwa  mwenyekiti  Mtendaji wa Bongo5 Music Group, Luca Neghesti.
Washndi wa tuzo hizo za watu 2015 ni:
Mtangazaji wa redio anayependwa- D’Jaro Arungu – TBC FM.
Kipindi cha redio kinachopendwa- Papaso – TBC FM.
Mtangazaji wa runinga anayependwa– Salim Kikeke (BBC Swahili)
Kipindi cha runinga kinachopendwa- Mkasi (EATV)
Blog/Website inayopendwa- millardayo.com
Muongozaji wa video anayependwa- Hanscana
Muongozaji wa filamu anayependwa- Vincent ‘Ray’ Kigosi
Muigizaji wa kike wa filamu anayependwa- Wema Sepetu
Muigizaji wa kiume wa filamu anayependwa- Hemedy PHD
Mwanamuziki wa kike anayependwa- Lady Jaydee
Mwanamuziki wa kiume anayependwa- Ali Kiba
Filamu inayopendwa- Kigodoro
Video ya muziki inayopendwa- ‘Nani kama Mama’– Christian Bella Feat. Ommy Dimpoz
TUOZ
Baadhi ya washindi wakiwa na tuzo zao, kutoka kushoto ni Msanii bora wa kike, Lady Jaydee akifuatiwa naa Ommy Dimpoz. anayefuata ni dada wa mwanamuziki Ali Kiba aliyempokelea tuzo kwa niaba yake akifautiwa na Millard Ayo.
TUWmwenyekiti  Mtendaji wa Bongo5 Music Group, Luca Neghesti ambao ndio waandaji wa tuzo hizo akielezea machache kwenye redcarpet juu  ya tuzo hizo na kituo cha About Bongo.com ambao ni Online TV.
YY
‘crew friends’ marafiki KN na NS wakiwa pamoja na marafiki zao katika redcarpet katika tukio la utoaji wa tuzo za watu 2015
TZ
Mtangazaji wa  radio ya Taifa ya TBC FM, Djaro Alungu ambaye aliibuka na tuzo mbili kwa mwaka huu na kuvunja rekodi ya aliyekuwa mtangazaji mwenzake, Millard Ayo,  akiwa na tuzo zake pamoja na crew yake.
DSC_0848
Mtangazaji wa BBC SWAHILI, wa Dira ya Dunia, Salm Kikeke akitoa nasaha kwa waliofika wakati wa kupokea tuzo yake hiyo,
20150504101541 - Copy
Mwanamuziki Ommy Dimpoz akiwa katika pozi na Andrew Chale, Mwandishi Mwandamizi wa Mtandao huu wa Modewjiblog.com muda mfupi baada ya kupokea tuzo yake.
IMG_20150522_193013Baadhi  ya warembo waliopamba usiku huo wa tuzo za watu 2015 chini ya usimamizi wa Ally Rehmtullah (katikati) wakiwa katika pozi..

No comments:

Post a Comment