Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, February 27, 2015

LIVERPOOL NA TOTTENHAM ZATUPWA NJE UEFA EUROPA LEAGUE. EVERTON YASONGA


Mechi za Marudiano za Raundi ya Mtoano ya Timu 32 za EUROPA LIGI zimechezwa Usiku huu na Klabu za England, ukiondoa Everton ambayo imeshinda Mechi zao zote mbili kwa kishindo na kufuzu, Tottenham na Liverpool, zote zimetupwa nje pamoja na Celtic ya Scotland.
Wachezaji wa Besiktas wakishangilia huko Uturuki leo
 Liverpool, ambao walishinda Mechi yao ya kwanza huko Anfield Wiki iliyopita, Leo wamechapwa Bao 1-0 na Besiktas huko Uturuki na Mechi kwenda Dakika 30 za Nyongeza lakini Matokeo yakabaki hivyo hivyo na ikaja Mikwaju ya Penati 5 na Besiktas kushinda 5-4.
Dejan Lovren ndie aliekosa Penati muhimu ya Liverpool. 
Dejan akipagawa baada ya kukosa mkwaju wa penati muhimu...Umetukosesha ulaji Kijana!!Dejan akiwaza!!Daaa!!! leo! mhhh!Nimekosa penati!!Demba Ba furaha tupu!!Wachezaji wa Besiktas wakishangilia huko Uturuki leoUshindi kwa Mikwaju ya penati!Mapema penati zikipigwa Wachezaji wa Liverpool wakijiaminia Tolgay ndie aliewafungia bao 1-0Sahan akishangilia baoPatashika kwa kipa wa Liverpool.
Nao Tottenham, wakicheza Ugenini baada ya Sare ya Nyumbani ya 1-1, walipigwa Bao 2-0 na Fiorentina huko Italy kwa Bao za Kipindi cha Pili za Mario Gomes na Mchezaji wa Chelsea Mohamed Salah.
Celtic, wakicheza Ugenini baada ya Sare ya Nyumbani ya 3-3 na Inter Milan, walitandikwa Bao 1-0 huko San Siro Milan, Italy kwa Bao la Freddy Guarin la Dakika ya 88.
Everton, ambayo ilipata ushindi mnono wa Ugenini Wiki iliyopita walipoichapa BSC Young Boys ya Uswisi Bao 4-1, Leo huko kwao Goodison Park wameitandika tena Young Boys Bao 3-1.
Bao za Everton zilifungwa na Romelu Lukaku, Bao 2 moja la Penati, na jingine la Kevin Mirallas huku Bao la Young Boys likifungwa na Sekoiu Junior Sanogo.

Nao Mabingwa Watetezi Sevilla wamesonga baada ya kuifunga Borussia Mönchengladbach 3-2 huko Germany na hiki ni kipigo cha Pili kwa Wajerumani hao baada ya pia kuchapwa 1-0 katika Mechi ya Kwanza.
Washindi wa Raundi hii watajua Wapinzani wao Raundi ya Mtoano ya Timu 16 wakati Droo ya Mechi zao itakapofanyika Leo Ijumaa Mchana huko Nyon, Uswisi.The last 16 are: EVERTON, Ajax, Besiktas, Club Brugge, Dinamo Moscow, Dnipro, Dynamo Kiev, Fiorentina, Inter Milan, Napoli, Roma, Sevilla, Torino, Villarreal, Wolfsburg, Zenit St Petersburg.

No comments:

Post a Comment